FAHAMU MAMBO MUHIMU YAPATIKANAO KATIKA UFUGAJI WA SAMAKI

Image result for UFUGAJI WA SAMAKI


UTANGULIZI
 Ufugaji wa samaki unakua kwa kasi sana hapa nchini tanzania kutokana na kuonekana kua na faida sana. hivyo nimeamua leo nikupe elimu kidogo ambayo itakusaidia wewe mfugaji ambaye ungependa kujikita katika ufugaji huo, hivyo tue pamoja ili kujua mengi.
SIFA ZA ENEO LA KUFUGIA SAMAKI
Sio kila mahali hufaa kwa ufugaji wa samaki, ila mahali ambapo ni sahihi, zifuatazo ni sifa za eneo bora la kufugia samaki.
  • eneo linalo fikika kwa urahisi
  • eneo tulivu na lenye usalama wa kutosha
  • eneo ambalo linavibali vyote vya umiliki
  • lazima liwe na maji ya kutosha kwa kipindi chote utakacho fuga
  • eneo ambalo halina mmomonyoko wala historia ya mafuriko
  • eneo lenye uwezo wa kutuamisha maji
  • eneo ambalo soko lake sio la shida
UTENGENEZAJI WA BWAWA
Kuna aina mbali mbali za kutengeneza mabwawa ya samaki inategemea na eneo, kiasi cha samaki unao taka kufuga, aina ya samaki na hali ya uchumi.

aina hizo ni
  • bwawa la kuchimba udongo bila kujengea(earthen pond)
 
  • bwawa la kuchimba na kujengea 
 
 hivyo unaweza kuchangua kulingana na sifa nilizo taja hapo mwanzo
 UPANDIKIZAJI WA VIFARANGA/MBEGU ZA SAMAKI KATIKA BWAWA
Kabla vifaranga hawaja safirishwa ni vyema kuwatoa katika bwa kubwa wanalo ishi na kuwaweka katika vibwa vidogo vidogo  kati ya masaa 24 hadi 72 kuendana na umbali wa safari bila kuwapa chakula chochote kile.
  • baada ya kuwasafirisha mfugaji  atakiwi kuviweka kwenye bwa moja kwa moja ila inatakiwa maji yalio tumika katika kuwasafirisha yabadilishane joto na maji ya bwawa ambalo wataenda kuishi. hivyo mfugaji anatakiwa kuliweka kontena ambalo vifaranga wamo ndani ya bwawa ambalo wataishi kwa dakika 30 hadi 35 bila kuwafungulia, baada ya hapo kontena liina mishwe taratibu ili kuwezesha maji ya bwawa na yaliyo kwenye kontena kubadilishana na baadae vifaranga watatoka taratibu,
endapo hautafanya hivyo  unaweza kusababisha vifaranga vyote kufa kutokana na mabadiliko   ya joto ambayo yanaweza kutokea ghafla.
  • unatakiwa kusafirisha vifaranga wako mda ambao hali ya hewa inakua sio joto yaan mda wa jion na asubuhi ili kuwezesha vifaranga kuimili misukosuko ya safari na bila kupatwa na joto kali.
CHAKULA NA UTUNZAJI WA SAMAKI BWAWANI
  • Samaki hutakiwa kupewa chakula angalau mara 2 kila  siku  unatakiwa kuzingatia mda sahihi wa kuwapa chakula yaan asubuhi saa 3-4 na jion saa 9 -10 samaki upewa vyakula tofauti kulingana na aina. 
tabia ya ulaji wa samaki ni kama ifuatavyo 
  1. samaki wanao kula nyama (sangara, kambale)
  2. samaki wanao kula mimea carps
  3. samaki wanao kula mchanganyiko (perege,sato na samaki wa maji ya chumvi mfano kibua)
zingatia kuweka maji  ambayo ni safi 
TARATIBU ZA ULISHAJI WA SAMAKI
UMRI(wiki)                          UZITO(gm)             KIASI CHA CHAKULA KWA SIKU (gm)
1-2                                           5-10                                   1
2-3                                           20-50                                 2
3-5                                           50-110                              3
5-7                                            110-200                           4
7 nakuendelea                          200 na zaidi                     5

Hakuna maoni:

CHANGE LANGUAGE

Inaendeshwa na Blogger.