VISABABISHI AMBAVYO VINAWEZA KUCHANGIA KUKU WASITAGE VIZURI



​Nawasalimu Nyote​
​Karibu Tuvijue Visababishi Ambavyo Vinaweza Kuchangia Kuku Wasitage Vizuri:-​
​1.​ Kuku wasipopewa chakula kwa wakati, chakutosha na bora (balanced diet).

​2.​ Joto Likiwa Kali (Heat Stress). Hili huwapunguzia hamu ya kula na pia kuku hutumia nguvu nyingi kupambana kupunguza joto.

​3.​ Kuku wasipopata mwanga wa jua na majani ya kutosha.

​4.​ Minyooo. Minyoo hutumia sehemu kubwa ya chakula kinacholiwa na kuku hivyo kusababisha utagaji na ukujua kua duni.

​5.​ Msongamano wa kuku bandani (Overcrowding).

​6.​ Chakula Kuwa Na Protein Nyingi Ambayo Hufanya Miili Yao Kujaa Mafuta Inasababisha Wasitage pia.

​7.​ Baridi huachangia kuku kupunguza kutaga vizuri kwasababu wanatumia nguvu nyingine kujikinga na baridi kwaiyo utagaji unakua sio mzuri.

​8.​Magonjwa mfano wa Typhoid, Ugonjwa wa kuhara damu (Coccidiosis) nk.

​Tufanyeje Nini Kuzikabili Hizi Changemote​
​1.​ Kuku/ndege wapewe chakula chakutosha, kwa wakati na chenye viinilishe vyote muhimu(balanced diet).

​2.​Hakikisha Kuku wako wanapata chanjo zote muhimu na dawa za minyoo kila baada ya miezi ​3​.

​3.​ Hakikisha Kuku wanapata mwanga wa kutosha na majani.

​4.​ Kuku wapate nafasi ya kutosha bandani

 


                ​

Hakuna maoni:

CHANGE LANGUAGE

Inaendeshwa na Blogger.