JINSI YA KULEA VIFARANGA VYA NDEGE mfano vifaranga vya kuku na bata.

 JINSI YA KULEA VIFARANGA WA KUKU

➡️Hakikisha banda la vifaranga pamoja na vyombo umepuliza dawa ya kuua bakteria kwa kutumia dawa ya VRID nk kabla hujaingiza vifaranga.    
➡️Hakikisha unavifaa vya joto (a) kama unatumia umeme au solar tumia Balbu, heater, modules nk.   (b) kama umeme huna tumia chemli, karabai, jiko la mkaa, vidumu vya maji ya moto, vyungu vya joto.      
➡️Baada ya hapo kuanzia siku ya 1-5 wape Grucose(glucovent ya ndege) + Otc plus/chicken plus + vitamin either ununue Multivitamin/vitalstress                      ➡️Wakitimiza siku ya 7 wape chanjo ya Newcastle deases(mdondo) then uendelee kuwapa Vitamins                    ➡️wakitimiza wiki 2 yaan siku 14 zikiisha wape chanjo ya gomboro(uendelee na maji ya vitamins.                             ➡️wakitimiza wiki 3 utarudia chanjo ya  mdondo na kuwapa                      
➡️Wakitimiza wiki 5 wape chanjo ya Ndui(fowlpox)  pamoja na dawa ya minyoo kama Ascaress( piperazine)                                                                    
➡️Chakula cha vifaranga kuanzia siku ya 1 mpaka wiki ya 8 wape either sterter / chick mash na kuanzia miezi 3-4 wape Chakula aina Growers /finisher nk.                                          ➡️wakifikisha wiki ya 16  kata midomo kisha wape Neoxyvital mfululizo kwa muda wa siku 4-6.                 ➡️usafi wa banda na vyimbo ndo nguzo ya msingi hakikisha kila baada ya miezi 3 unapuliza dawa kuuwa bakteria kama   VRID  pia zingatia muda sahihi wa madawa kwa magonjwa yote ya kuku iwe ya Virus, Bakteria nk pia maji safi ni muhimu kitaalamu kuku mmoja hunywa maji robo litre na gram 125/150 za chakula per day  so ukizingatia hvyo hakika utaona mafanikio ya ufugaji acha kufuga fuga kibiashara   nitaendelea. Ahsanten nakaribisha maswali na nyongeza kwa watalaamu wengine wadau
Kanuni kumi sahili za kuzuia magonjwa katika ndege (kuku, bata, bata mzinga, kanga) Wape kuku lishe jnayofaa na maji safi haswa vifaranga wadogo. Wajengee mabanda ya mazuri ya kujisetiri dhidi ya upepo na mvua. Safisha banda/nyumba ya ndege mara kwa mara. Ikiwa ni lazima wapatie takataka kavu mara kwa mara. Usiweke ndege wengi pamoja. 6. Aina tofauti za ndege kwa mfano kuku,bata mzinga na bata wanafaa kutenganishwa. 7. Watenganishe vifaranga na ndege wakubwa ila tu kwa mama yao. 8. Chanja vifaranga dhidi ya magonjwa muhimu na wachanje mara tena ikikulazimu. Kumbuka ni ndege tu walio na afya bora wanafaa kuchanjwa. 9. Watenge ndege wagonjwa-ikiwa matibabu hayapatikani waue ndege wagonjwa. 10. Choma ama zika ndege waliouliwa.

JINSI YA KULEA VIFARANGA WA BATA MZINGA.

Vifaranga Wa bata mzinga ni tofauti na Wa kuku wakuku hutotolewa tayari wanajua kujifunza kula na kunywa Maji wakati Wa bata mzinga huzubaa kwa siku kama 4 ndipo wajue kula vizuri hivya wana hitaji uangalizi Wa hali ya juu sana.<brHukaa kwenye brooder kwa muda Wa wiki 4 ambapo watahitaji joto la kutosha muda wote ambapo wiki ya kwanza watahitaji nyuzi joto 38 na na wiki ya pili utapunguza nyuzi joto 5 kila wiki utapunguza nyuzi joto 5.wanakuwa kwa haraka hivyo wanahitaji sehemu Kubwa ya kuwalea sentimita 20x20 kwa kila kifaranga kwenye wiki ya pili hadi ya Tatu. Wanahitaji Chakula chenye protini nyingi 28% ktk Chakula chao kwa wiki 8 za mwanzoni hivyo ni bora kuwapa broiler starter kwa muda Wa miezi miwili. Maharisho ya sehemu ya kuwale (brooder) yanatakiwa yazingatie mambo yafuatayo: Kuwe kuna matandiko chini ya kutosha kiasi cha kina cha inch 3 ili kuweka hali ya joto. Matandiko yaweza kuwa maranda nyasi pumba za mpunga. Weka vyombo vya kulia Chakula na kunywea Maji kabla hujawaingiza Vifaranga hao. Weka vitu vya kung'aa ktk Chakula na Maji ili kuwa vutia kujifunza kula. Vitu vya kung'aa yaweza kuwa gololi zile za kuchezea watoto unatumbukiza kwenye Maji hivyo zile Rangi zitawavutia kusogea pale na kudonoa donoa au weka Maji ya Mchele km Maji yao ya kunywa ile Rangi nyeupe itawavutia kusogelea Maji hii ni namna ya kuwafunza kula au wachanganye na Vifaranga Wa kuku watajifunza kula kupitia Vifaranga Wa kuku. Wape Chakula muda wate na wape Majani wiki ya pili maana 50% ya Chakula chao ni Majani Mboga Mboga mbichi. Wape joto kwa vyanzo vya joto ulivyo navyo kama taa za umeme 100w au 200w jiko la Mkaa taa ya chemli au kandiri au tumia Njia za asili. Kama ilivyo kwa kuku bata mzinga wanahitaji Dawa na chajo Wiki ya kwanza wape Newcastle vaccine wiki ya 4 wape fowl pox vaccine (ndui) wiki ya 6 wape Newcastle vaccine Utarudia baada ya miezi mitatu mitatu chanjo hii ya Newcastle. Wape vitamini na madini ktk Chakula chao. Ikifika wiki ya 8 unaweza kuanza kuwatoa nje wajifunze mazingira ya nje na kujitafutia maana bata mzinga ni wajitafutiaji Chakula wazuri km kuku Wa kienyeji japo hupenda sana Majani. Ni vizuri kuwapa lusina mbichi hufanya vizuri ktk bata mzinga. Wiki ya 24 hadi 28 wanakuwa tayari wana kilo 8 hadi 12 hivyo wanaanza kutaga wachanganye na maduma katika ratio ya 1:5 yani dume 1 majike 5 hii ni kama bado hawajawa wazito sana kama wameshakuwa wazito au kuanze kuwa wavivu kuzeeka wawekee ratio ya 1:3 yani dume 1 majike 3. Bata mzinga hutaga kwa msimu kama walivyo kanga na hulalia siku 28 kama kanga na wanauwezo wakulalia Mayai yao 10 hadi 15 lakini hutaga mengi zaidi hivyo nivizuri ukatumia Mashine ya kutotolesha au kama una kuku Wa kienyeji anapo lalia unamuwekea ya bata mzinga Mayai 6. Hivyo wakati huo bata anaendelea kutaga huku kuku wanalalia Mayai yao. Hivyo ni Njia nzuri maana bata mzinga wanatabia ya kususa Mayai yao km MTU ukiyashika na marashi au yakipata harufu ambayo sio yake.Lakini kukuza vifaranga ni zoezi rahisi na linalowezekana kama utakubali kuvifuatilia kwa karibu. Kitu cha kwanza kabisa unahitaji kuvitenga vifaranga viweke kwenye chumba na kuhakikisha vinapata joto la wastani. Njia nzuri na isio na gharama kubwa yakutengeza joto ni kwakutumia jiko la mkaa liwashe nje likisha waka vizuri liingize kwenye chumba chao. Ni rahisi kutambua kama joto linawatosheleza ama la. Joto linapokua kali utawaona vifaranga wakiachama midomo kama vile afanyavyo mbwa pia hutanua mbawa zao na kuachiana nafasi ukiona hivyo fungua madirisha kwa muda mpaka wawe kwenye hali ya kawaida kisha funga tena madirisha ili kuhifadhi joto kuokoa matumizi ya mkaa mara kwa mara. Joto linapopungua vifaranga hukusanyana hapo tambua kwamba wanasikia baridi hivyo ingiza jiko ndani. Njia hii yakutumia jiko ni rahisi kwani kama utawasha jiko usiku saa mbili hutaweka tena mpaka asubuhi cha msingi chumba kisiwe na upotevu wa joto Jambo la pili ni ma.
Hakikisha unawapatia vifaranga wako chanjo ya new castle(Mdondo/Kideri),Fowl pox(Ndui) na chanjo ya Gumboro(Mbande).

Jambo la nne ni matumizi ya dawa zenye mult vitamin  vitamini hutumika wakati wote kwani husaidia kuwapa vifaranga vitamini pia huviongezea nguvu.
Jambo la tano ambalo pia ni muhimu ni kuvipa vifaranga vyakula venye mchanganyiko maalumu walau kwa miezi miwili.Vyakula hivi vinauzwa madukani lakini pia kama unaweza na kuelewa mchanganyiko huo unaweza fanya mwenyewe.




Hakuna maoni:

CHANGE LANGUAGE

Inaendeshwa na Blogger.