UFUGAJI WA SAMAKI


Kuna aina nyingi za samaki wa maji baridi ambao wanaweza kufugika kwaurahisi au ugumu kidogo tu na aina hizo wapo wale ambao sio wakuzaliana(monosexual) na wale wa kuzaliana(heterosexual)
Urahisi hapa uko zaidi kwenye kuwafuga wasiozaliana sababu hawaongezekiwakati wale wanaozaliana utakuwa na utaratibu wa kuhamishafishling(vifarangasehemu nyingine.
Rasilimali muhimu za kuwa nazo ili kufanikisha shughuli hii ni eneo laardhi,majirasilimali watu na rasilimali fedha.Eneo la ardhi ndio litakaloonyeshani kwa namna gani bwawa lako liwe,aidha la kujengea na cement,kutandikaplastic au kuchimba na kulitumia hivyohivyo.Bwawa huchimbwa/kujengwa kwa kuwa na sakafu yenye ulalo kiasi(gentle slope/gradient)
Wapo samaki aina ya Sato(Tilapia),Kambale(African catfish) na wengine ainaya pangasius ambao hufugwa kwa wingi sana.
Unahitaji samaki 7-8 katika meter moja ya mraba(1m^2) ,kwa maana hiyokama una meter za mraba 600 nasi unaweza kufuga samaki 4500.Haishauriwikulundika samaki kwenye eneo dogo kwani itawasababishia ukosefu wahewa(oxygen).Ingawa zipo njia za kuweza kuongeza upatikanaji wa hewakwenye mabwawa.
Ukishachimba bwawa lako(aidha na kulijengeaunaingiza maji kwenye bwawahakikisha yamekaribia futi 2.5 mpaka kujaa full.Itakubidi kufanyaliming(kumwagia chokaa bwawa kabla ya kuweka maji ili kuua bacteriahatarishi kwa maisha na afya ya samaki wako) pia unahitajika kuyarutubishahayo maji kwa kuchanganya na mbolea(kama ya ng’ombe na za viwandani piaingawa haishauriwi sana) na kusubiria kwa muda usiopungua siku 21 auzaidi.Unafanya hivi ili kuweka mazingira ya chakula asili(natural foood) kwa ajiliya samaki kujitengeneza,vyakula hivo hua katika hali ya mimea na viumbewadogo(microorganisms)
Upatikanaji wa vifaranga vya samaki,hapa inakubidi uwe makini sana kamaumeamua kuzalisha sato,changamoto kubwa ya sato ni kupata mbeguambayo under right conditions vifaranga vitaweza kua samaki wenye uzito wakutosha(miezi 6 awe at least 500grams au zaidi).Mbegu ya sato hupatikanakwa bei rejareja ya sh 300 na kambale sh 500 kwa kifaranga kimoja.Wapowazalishaji wengi wa mbegu za vifaranga wa ndani na nje ya nchi ila kwa Tanzania nimewakubali Tanzania Fisheries Research Institute(TAFIRI)Nyegezi,Mwanza
Ulishaji wa vifaranga vyako ,chakula chao kinategemea na uzito wao mfanosamaki hula 5% ya uzito wake wa mwili akiwa mdogo na 3% akiwamkubwa.Hapa tunaongelea ulishaji wa chakula cha ziada(supplement food),sababu cha asili amekipata kwenye ile mbolea ulioweka.Kama unavifaranga 100 vyenye gram 10 kila kimoja basi utahitaji gram 50 kuwalisha.
Itakuchukua Miezi 6-9 kuanza kuvuna samaki wako ambao unaweza kuwauzakulingana na uzito au au njia utayoona inakufaa.Samaki wengi wa kwenyemabwawa wanavunwa kwa kutumia nyavu au kumwaga maji yote nje yabwawa.Masoko yake haya samaki ni pamoja na supermarkets,wafanyabiashara sokoni na mitaani pamoja na watu binafsi.
By Ufugaji kwa maendekeo

Hakuna maoni:

CHANGE LANGUAGE

Inaendeshwa na Blogger.